Header Ads 728*90

MIAKA 43 NA SIKU 5 UNITED YAFUFUKA TAFF MORE.


Na John Richard
USISHANGAE  hii ni kawaida kwa Manchester United kuvunja rekodi, na kuandika rekodi, naimani utakubaliana na mimi ukimkumbuka Sir Alex, alifanya mengi sana na kuandika historia nyingi sana, Jose Mourinho anakuja United anaandika historia ya kufunga bao kunako uwanja wa Taff More, nyumbani kwa Burnely.

Antonio Martial aliyeiandikia united bao la kwanza kunako dakika 21, baaada kuanzisha kaunta ataki na ander herera kumpasia Martial na kupachika bao la kwanza kwa United, alikuwa tena Martial aliyepiga pasi ya mwisho kwa Wayne Rooney na kupachika bao la pili kunako dakika 39, hadi mapumziko Burnely 0-2 Manchester United.



Haikuwa historia tu kwa United kufunga bao kwenye uwanja wa Taff More, baada ya miaka 43 na siku 5, Antonio Martial anaandika historia kwenye mchezo huo kwa kufunga bao lake la kwanza na pasi ya bao nje ya uwanja wa Old Trafford, kunako ligi kuu ya Uingereza toka atue Uingerza kuichezea United. 

No comments

Powered by Blogger.