Header Ads 728*90

BARCA YAPOOZA MAUMIVU YA JUVE KWA MADRID

Na John Richard
BAADA ya mabingwa mara tano wa Uefa champion leage, Barcelona kuondoshwa na vibibi kizee vya Torino katika hatua ya robo fainali, wamehamishia hasira zao kunako Laliga kuusaka uchampioni huo kwa ali na mali.

Barcelona iliingia uwanjani ikiwa nyuma point 3 mbele ya mahasimu wao Real Madrid ambao wana faida ya mchezo mmoja mkononi na bado wamefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali katika michuano ya Uefa Championi Leage hali inayo wafanya kuwania makombe mawili msimu huu.
Madrid walikuwa wanahitaji ushindi katika mchezo wa jana ili kujihakikishia nafasi ya kutwaaa ubingwa wa Ligi kuu ya Hispania alimaarufu kama Laliga walioukosa kwa takribani misimu mine iliyopita.

 Alikuwa Casimiro aliyeiandikia Madrid bao la kwanza kunako dakika ya  na Lion Mess kuisawazishia Barcelona kunako dakika ya hadi mapumziko Real Madrid 1 Barcelona 1. Licha ya mchezo huo kuwa wavuta nikuvute kwa pande zote mbili.

Kunako kipindi cha pili timu zote zililejea huku kila timu ikionekana kuwa na mipango mingi ya kutafuta mabao, Latcht alikuwa shujaa kwa kuwainua mashabiki wa Barcelona kwenye viti vya Santiago Bernabeu kwa mara ya pili.

James Rodriquez super sub, anaisawazishia Madrid bao la pili kunako dakika ya 86, aliyeingia baada ya Madrid kupata pigo la kutolewa kwa Sergio Ramos kwa kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo huo kwa kudhani kuwa amemchezea Lion Mess lafu.

Hadi dakika 90 za mchezo huo mashabiki wa Madrid wanaamini kubaki na point moja na kuendelea kuongoza juu kwa point 3 zaidi, Lion Mess anapachika bao la 3 likiwa la pili kwake katika mchezo huo.

Barcelona wanashika usukani wa ligi kuu ya Hispania kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa  wakiwa na point 76 sawa na Real Madrid wenye point 76, Madrid wanafaida ya mchezo mmoja mkononi.

No comments

Powered by Blogger.