Header Ads 728*90

CHIRWA AITAKATISHA YANGA TAIFA

Na John Richard
Mshambuliaji wa klabu ya yanga obrey chirwa ameongeza matumaini ya kutetea ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara kwenye klabu yake baada ya kuifungia bao la ushindi katika mchezo uliopigwa jana kunako uwanja wa taifa jijini dare s salaam.

Haikuwa rahisi kwa wana wa jangwani kuibuka na ushindi katika mchezo huo, ambao walionekana kuzidiwa kimbinu na wapinzani wao Azam Fc,
Timu zote zilicheza kwa umakini mkubwa huku azam walionekana kuutawala mchezo takribani dakika 70, na kutengeneza nafasi nyingi ambazo washambuluiaji wake hawakuweza kuzitumia vyema


Kunako dakika ya 70, Obrey Chirwa aliweza kuwatoka mabeki wa Azam nq kuweza kupachika bao ambalo liliifanya yanga kuondoka na ushindi katika mchezo huo na alama tatu muhimu, ambazo zinaifanya yanga kukaa kilelelni kwa muda wa masaa 24 kabla vinala wa ligi hiyo Simba kushuka uwanjani masaa machache yajayo kunako dimba la kaitaba kuivaa kagera sugar.  

No comments

Powered by Blogger.