Header Ads 728*90

YANGA YAIPANDIA SIMBA KILELENI



Na John Richard
LIGI kuu Tanzania bara (VPL) imeendelea hapo jana na kushuhudia mchezo kati ya Yanga dhidi ya Azam, na Yanga kuibuka na alama tatu muhimu, mchezo uliopigwa uwanja wa taifa jijini dar es salaam.

Haikuwa rahisi kwa Yanga kuibuka na ushindi katika mchezo huo, kwani Azam walionekana kuutawala mchezo takribani dakika 70, licha ya kupoteza nafasi nyingi za wazi.
Alikuwa Obrey chirwa alipotumia vyema makosa ya mabeki wa  Azam kwa kushindwa kuwa na mawasiliano mazuri na kipa wao, baada ya kupoteza mpira na kumkuta Chirwa kunako dakika ya 70 na kupachika bao lililodumu hadi dakika 90 za mchezo kumalizika.
Yanga waliingia kwenya mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kipigo cha bao 4-0, walichokipata walipokutana na Azam kwenye kombe la Mapinduzi mwezi January mwaka huu huko Zanzibar.

No comments

Powered by Blogger.