Header Ads 728*90

MC' PILIPILI ATOANSOMO KWA VIJANA WENYE VIPAJI



Na John Richard
JINA la Emmanuel Mathias MC’ Pilpili’ hakika limezidi kuwa Lulu katika sherehe mbalimbali katika jamii ya kitanzania, hii ni kutokana na kipaji chake cha ushereheshaji alichojaliwa na Mwenyezi Mungu.

Kupitia kipaji chake cha ushereheshaji MC’ Pilipili amejizolea umaruufu mkumbwa miongoni mwa watanzania walio wengi na kufanya thamani ya kazi yake kuwa juu kila uchao.

MC’ Pilipili kupitia uchekeshaji na ushereheshaji ameweza kuvuka mipaka ya Tanzania kwa kwenda Kenya, Uganda, Rwanda pamoja na Afrika ya kusini safari ambazo zimemfanaya ajitangaze zaidi na kufahamika nje ya mipaka ya Tanzania.

Akizungumza na Wanafunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari (TSJ), katika sherehe ya Bash iliyofanyika tarehe 7, mwezi huu, katika viwanja vya Water World, Kunduchi Jijini Dar es Salaam, MC’ Pilipili alisema alipenda kuwa mwandishi wa habari angali yupo shule ya msingi lakini Mama yake alikuwa kikwazo.

“Nilipata   wakati mgumu sana kufanya uamuzi kwani  nilipenda kuwa Mwandishi wa habari na wakati huo huo mama yangu alisisitiza niende ualimu kwani hata katika familia yetu hakuna hata mmoja aliyewahi kuwa mwandishi wa habari,”.Alisema MC’

Hakika uwepo wake katika Bash hiyo uliwafanya wote waliohudhuria kuona hawakukosea kujumuika katika tukio hilo la Bash ambalo huandaliwa na Serikali ya Wanafunzi Chuoni hapo kila mwaka.

Licha ya kunogesha sherehe hiyo alitoa Sh, Laki mbili za Kitanzania kwa kuinunua Keki iliyoandaliwa na Serikali ya Wanafunzi (TISJOSO), sambamba na kiasi hicho cha fedha alichokitoa, pia aliahidi kununua kompyuta moja kwa ajili ya Chuo.

MC’Pilipili akiwaasa wanafunzi wa TSJ, na vijana wa kitanzania kutumia vipaji vyao na sio kulazimisha vitu ambavyo ni vigumu kama vile kusoma, Alisema..

“Kipaji kinaweza kukupeleka mbele yawakuu” akitolea mfano wa watu wa kwenye Biblia kama Mfalme Daudi na Yusuph ambao walitumia vipaji vyao na wakainuliwa na Mungu.

“Napenda kutumia usemi unaosema ‘Sherehe ni Mc”. Aliyasema hayo akiwashauri washereheshaji wenzake kufanya kazi hiyo kwa kuhakikisha wanasoma vitabu, kuangalia intenet kuona nini wanatakiwa kufanya ili wafanye kazi hiyo katika kiwango kizuri.


 Pia anaishauri serikali kurudisha masomo ya sanaa na kuweka walimu maalum wanaojua sanaa kwa viwango na ubora unaoendana na ulimwengu wa teknolojia tuliyopo sasa.

No comments

Powered by Blogger.